Tuesday, May 8, 2012

DKT BILAL ATAKA JITIHADA ZAIDI KUPUNGUZA UMASIKINI NCHINI



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akizindua rasmi Jukwaa la Uchumi wa Kijani, litakaloendelea kwa siku tatu Mkoani Iringa. Uzinduzi huo umefanyika leo Mei 8, 2012, katika Ukumbi wa Shule ya Msingi Mtakatifu Dominic Savio, mkoani Iringa. Picha na Muhidin Sufiani-OMR




MAKAMU wa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mohamed Gharib Bilal jitihada zaidi kufanyika ili kupunguza kasi ya umasikini katika jamii nchini.

Alisema kuwa ili kuharakisha maendeleo nchini jitihada za makusudi za kupunguza umaskini na kuleta maendeleo lazima zifanywe kwa kuzingatia uhalisia wa mambo ikiwa ni pamoja na kulenga wakazi na uchumi kwa wananchi wa vijijini.
Makamu wa Rais aliyasema hayo mjini Iringa leo wakati akizindua jukwaa la Uchumi wa Kijani jana katika ukumbi wa St.Dominic Savio .

Dkt Bilal alisema kuwa upo uhusiano mkubwa kati ya watu maskini hasa wa vijijini na mazingira kutokana na watu wa vijijini huishi karibu na mazingira ya asili na hutegemea rasilimali za ardhi, maji na misitu kwa maisha yao.

"Mara nyingi matumizi hayo yamezisababishia hasara jamii ikiwa ni pamoja na upotevu wa maisha na kipato"




Alisema kuwa pamoja na kuzungumzia uharibifu wa mazingira unaofanywa vijijini bado ni tatizo na hakuna budi jamii kuendelea kuelimishwa zaidi .

Bilal alisema kuwa, masuala ya mazingira mijini pia ni muhimu kuzingatiwa kutokana na maeneo mengi ya miji hukabiliwa na changamoto za ubadilishaji wa matumizi ya ardhi kunakoendana na ukataji wa miti, uchimbaji mawe na pia ukaushaji wa ardhioevu kwani mambo hayo huchangia kwa kiasi kikubwa katika mabadiliko ya tabia ya nchi.




Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI Profesa Joseph Semboja alisema kuwa amepata faraja kuona idadi kubwa ya watunga sera, watoa maamuzi na viongozi mbalimbali wamedhibitisha kushiriki katika uzinduzi wa jukwaa la uchumi wa kijani.



Alieleza kuwa ukuaji wa uchumi endelevu ndio njia pekee ya kufikia ustawi wa kudumu kwani jukwaa hilo linalengo la kutoa njia madhubuti kwa viongozi wa serikali, sekta binafsi na asasi za kiraia pamoja na wote watakaochagua kufuata mkondo huo.


Aidha Naibu waziri wa kilimo, chakula na ushirika Adam Malima ameahidi kutoa ushirikiano kwa tasisi hiyo ili kukabiliana na tatizo la uharibifu wa mazingira ambao unapelekea mabadiliko ya tabia ya nchi.

kupata habari za sasa Bofya hapa

FAN CITY LODGE IPO MANISPAA YA MTWARA /MIKINDANI NI LODGE BORA YENYE HADHI ZAIDI

Furahia usiku wako ndani ya Fan city lodge ipo Manispaa ya Mtwara/Mikindani Maeneo ya Rahaleo jirani na ofisi za TRA mkoa waMtwara
Ni Lodge ya kisasa mtwara /Mikindani ukifika utaipenda zaidi
Mwonekano mzuri wa Lodge hii ni heshima kubwa kwa thamani ya fedha zako
Kila mmoja hufurahia huduma zetu ukifika hapa hutapenda kufikia Lodge nyingine uwapo Mtwara
Huduma za za mazoezi(GYM) pamoja na INTERNET wakati wote uwapo ndani ya chumba chako
Vitanda ni vya kisasa hakuna mfano
Fan city lodge ipo Manispaa ya Mtwara/Mikindani Maeneo ya Rahaleo
jirani na ofisi za TRA mkoa waMtwara

Wanatoa huduma za malazi,chakula na Usafiri wa ndani na nje ya
mkoa ni pacha na Naf Blue view hotel

huduma za za mazoezi(GYM) pamoja na INTERNET wakati wote uwapo lodge

Waweza kuwasiliana kwa namba
0652 295186 na 0788 030504
MTWARA...
WOTE MNAKARIBISHWA KUPATA HUDUMA BORA NA ZA KISASA ZAIDI SAWA NA MALIPO ULIYOTOA

Pata habari mpya hapa

Friday, May 4, 2012

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI HILI HAPA , LUKUVI APETA , MAKALA ,Dkt MAHENGE ,DKT MGIWA AULA

Rais Dkt Jakaya Kikwete
Mbunge wa jimbo la Ismani Iringa Wiliam Lukuvi ambaye ameachwa tena katika nafasi yake ya uwaziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera na uratibu wa bunge
mbunge wa jimbo la Makete mkoa mpya wa Njombe Eng. Dr. Binilith Mahenge, (kushoto) ambaye ameteuliwa kuwa naibu waziri wa maji akiwa na mkuu wa wilaya Dkt Norman Sigalla
Mbunge wa jimbo la Kalenga Dkt Wiliam Mgimwa aliyeteuliwa kuwa waziri wa fedha na uchumi leo ,hapa akisaini hundi kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa shule ya sekondari Lyandembela jimboni kwake
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE MicrosoftInternetExplorer4

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

ORODHA YA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI

MAWAZIRI

1. OFISI YA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)

Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)

Ndugu George Mkuchika, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)

Ndugu Celina Kombani, Mb.,

2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)

Ndugu Samia H. Suluhu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)

Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,

3. OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)

Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)

Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)

Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,

4. WIZARA

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,

Waziri wa Ujenzi

Dr. John P. Magufuli, Mb.,

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii

Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,

Waziri wa Katiba na Sheria

Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,

waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi

Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi

Dr. David M. David, Mb.,

Waziri wa Kazi na Ajira

Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia

Prof. Makame M. Mbarawa, Mb.,

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Prof. Anna K. Tibaijuka, Mb.,

Waziri wa Maji

Prof. Jumanne Maghembe, Mb.,

Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum

Prof. Mark Mwandosya, Mb.,

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika

Eng. Christopher Chiza, Mb.,

Waziri wa Uchukuzi

Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,

Waziri wa Maliasili na Utalii

Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,

Waziri wa Viwanda na Biashara

Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,

Waziri wa Fedha

Dr. William Mgimwa, Mb.,

Waziri wa Nishati na Madini

Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,

5. NAIBU MAWAZIRI

OFISI YA RAIS

HAKUNA NAIBU WAZIRI

OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais

Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,

7. OFISI YA WAZIRI MKUU

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)

Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)

Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,

8. WIZARA MBALIMBALI

Naibu Waziri wa Kazi na Ajira

Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika

Ndugu Adam Malima, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi

Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara

Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi

Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,

Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,

Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii

Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb.,

Naibu Waziri wa Ujenzi

Ndugu Gerson Lwenge, Mb.,

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,

Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb.,

Naibu Waziri wa Nishati na Madini

Ndugu George Simbachawene, Mb.,

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia

Ndugu January Makamba, Mb.,

Naibu Waziri wa Uchukuzi

Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,

Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

Ndugu Amos Makala, Mb.,

Naibu Waziri wa Maji

Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb.,

Naibu Waziri Nishati na Madini

Ndugu Stephen Maselle, Mb.,

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria

Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha

Ndugu Janet Mbene, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha

Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

4 Mei, 2012

Thursday, May 3, 2012

MISA TANZANIA NA TMF WALIVYOUNGANA KUSHEREKEA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI LEO
















































Press Release
May 2nd, 2012
Transforming societies central to 2012 World Press Freedom
Day celebrations
The Media Institute of Southern Africa (MISA) Tanzania Chapter in association with
the Tanzania Media Fund (TMF) are organising a World Press Freedom Day
commemoration event to be held at Mlimani City Hall on the 3rd of May, 2012.
The event is expected to start at 08:30am and is open to all journalists. Deputy
Speaker, Parliament of Tanzania Hon. Job Ndugai will bless the proceedings as the
guest of honor. This year’s celebration carries the theme ‘Media Freedom Helping to
Transform Societies’.
Among other things, the event will be marked with a dialogue that will focus on how to
transform Tanzanian media with presentations from some of the outspoken media
personalities; like Ayub Rioba from the School of Journalism and Mass
Communication (SJMC), Ms. Rosemary Mwakitwange from the East African Business
Centre, Ms Suzan Mungy, Director of Events at Tanzania Broadcasting Corporation
(TBC) and Social Affairs analyst Mr Deus Kibamba.
Stakeholders will discuss how the media industry in the country performs and suggest
solutions on how it can be improved in a way that can transform societies for the
better.
There will be testimonies from some of the journalists who have been victims of media
freedom violations and a book that contains articles on the state of media in Africa
South of Sahara, known as So This Is Democracy will be launched. Some of the
journalists and photographers will display their works.
2
Other stakeholders present will be members of the academia, government ministries
and agencies’ representatives, media owners, development partners and members of
parliament who are ardent users of the new media.
MISA-Tanzania (MISA-TAN) is one of the Media Institute of Southern African (MISA)
chapters established in 1997 as a non-governmental organization (NGO) under
society’s ordinance, 1954 with the major objective of promoting a free, independent
and pluralistic press in service of democracy, good governance and development in the
country.
One of the responsibilities of MISA-Tanzania is to publicize the WPFD commemorated
each year on May 3rd to recognize the role of free, independent and professional media
in promoting democracy and good governance, as expressed in Article 19 of the
Universal Declaration of Human Rights.
End.
Released by the information and research department
MISA-TAN

Kupata habari mpya zaidi bofya hapa

Thursday, April 12, 2012

BONGO MOVIE KUICHANGIA TWIGA STARS HEROES

Timu ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake (Twiga Stars) itacheza mechi ya kirafiki na timu ya wasanii wa filamu ya Bongo Movie itakayofanyika Jumamosi (Aprili 14 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
Lengo la mechi hiyo ya maonesho (exhibition) ni kuichangia Twiga Stars ambayo hivi sasa iko kwenye mashindano ya mchujo ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) ambayo fainali zake zitafanyika Novemba mwaka huu nchini Equatorial Guinea.
 
Pia asilimia mbili ya mapato yatakayopatikana kwenye mechi ya Twiga Stars na Bongo Movie yatakwenda kwenye familia ya mwigizaji nguli wa filamu Tanzania, Stephen Kanumba aliyefariki dunia Aprili 7 mwaka huu.
 
Kiingilio katika mechi hiyo kitakuwa sh. 10,000 kwa VIP A, sh. 5,000 kwa VIP C na B na sh. 2,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, kijani na bluu. Mechi itaanza saa 10 kamili jioni.
 
Twiga Stars itacheza mechi ya kwanza ya mchujo dhidi ya Ethiopia jijini Addis Ababa. Mechi hiyo itachezwa Mei 26 mwaka huu na wiki mbili baadaye timu hizo zitarudiana jijini Dar es Salaam. Twiga Stars ilifuzu raundi hiyo baada ya kuitoa Namibia kwa jumla ya mabao 7-2.
 
Machi 10 mwaka huu, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara alizindua akaunti ya Twiga Stars kupitia Tigo Pesa kuichangia timu hiyo ambayo inashiriki michuano ya AWC. Wachangiaji wanatakiwa kutuma mchango wao kwenda namba 13389.
 
 
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Kwa matukio ya Leo Leo ingia www.francisgodwin.bloodspot.com

Wednesday, April 11, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA CHUO CHA UFUNDI STADI CHA VETA MKOA WA LINDI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Balozi wa Korea nchini, Young-Hoon Kim, wakikata utepe kwa pamoja kuashiria uzinduzi rasmi wa Chuo kipya cha Ufundi Stadi cha VETA kilichojengwa Mkoa wa Lindi.Uzinduzi huo ulifanyika jana. Kulia ni Mkurugenzi wa VETA, Zebadia Moshi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akibonyeza 'Alam', kuashiria uzinduzi rasmi wa Chuo kipya cha Ufundi Stadi cha VETA kilichojengwa Mkoa wa Lindi. Uzinduzi huo ulifanyika jana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la Chuo cha Ufundi Stadi cha VETA baada ya kuzindua rasmi chuo hicho kilichojengwa Mkoa wa Lindi. Uzinduzi huo ulifanyika jana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akiongozana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Shukuru Kawambwa, Balozi wa Korea nchini, Young-Hoon Kim na Viongozi wa VETA, wakati akitembelea na kukagua baadhi ya majengo mapya yaliyojengwa ya Chuo cha Ufundi Stadi cha VETA, baada ya kuzindua rasmi chuo hicho mkoa wa Lindi jana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Ghariub Bilal,akisikiliza maelezo kuhusu jinsi ya ufundishaji wanafunzi kwa kutumia mtambo wa kufua Umeme, kutoka kwa Mwalimu wa Umeme Veta, Majolo Mwigole, wakati Makamu alipofika kuzindua Chuo hicho cha VETA mkoa wa Lindi jana. Picha na Muhidin Sufiani-OMR.

Kwa matukio mapya ya sasa bofya hapa